WANENGUAJI WAWILI WAHUKUMIWA JELA KWA KUKATA VIUNO WAKIWA NUSU UCHI




Mahakama nchini Misri imewahukumu wanenguaji viuno wawili kufungwa jela miezi sita kila mmoja kwa kuchochea uasherati.

Suha Mohammed Ali na Dalia Kamal Youssef, wanaojulikana kama Shakira na Bardis wa Misri, walikamatwa kwa kusakata ngoma katika video wakiwa nusu uchi.

Mawakili waliwasilisha malalamishi kortini, wakisema wawili hao walikuwa kero kwa umma kimaadili na waliwaharibia sifa wanawake wa Misri.

Mwezi Machi, mchezaji densi mwingine kwa jina Safinaz alifungwa jela miezi sita kwa kuikosea heshima bendera ya taifa hilo.

Alikuwa ametokea kwenye video akivalia nguo yenye rangi za bendera ya Misri.

Msakataji densi mwingine, Salma el-Fouly, alifungwa miezi sita mwezi Julai kwa kucheza kwenye video akiwa amevalia mavazi mafupi na kuonekana kuchezea waume.

Mwanamume aliyepiga picha hizo za video pia alifungwa jela miezi sita, huku mwanamume wa pili aliyetokea kwenye video hiyo na ambaye pia alihudumu kama produsa akihukumiwa mwaka mmoja jela bila yeye kuwa kortini.

Chanzo-BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527