Kumekucha CCM!! HII NDIYO KAMATI YA KAMPENI YA UCHAGUZI 2015 CCM YA WATU 32,YUMO MAKONGORO NYERERE,KINANA,NAPE,WASSIRA,JANUARY MAKAMBA,STEPHEN MASELE



Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa jana Agosti 17, 2015 katika kikao chake cha siku moja kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dokta Jakaya Mrisho Kikwete imekamilisha kazi ya uteuzi wa Wagombea Ubunge katika majimbo mawili ya Singida Mashariki na Kiteto.


Wagombea ubunge walioteuliwa kupeperusha bendera ya CCM katika majimbo hayo ni pamoja na Ndugu Jonathan Njau (Singida Mashariki) na Ndugu Emmanuel Papian John (Kiteto).

Aidha Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Kamati ya Kampeni kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 ambayo itaongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

Wajumbe wa Kamati hiyo ni kama ifuatavyo;-


1. Ndugu Abdulrahman Kinana - Mwenyekiti
2. Ndugu Rajab Luhwavi - Makamu Mwenyekiti – Bara
3. Ndugu Vuai Ali Vuai - Makamu Mwenyekiti - Z’bar
4. Ndugu Sofia Simba
5. Ndugu Mohamed Seif Khatib
6. Ndugu Asha-Rose Migiro
7. Ndugu Samwel Sitta
8. Ndugu Nape Nnauye
9. Ndugu Mwigulu Nchemba
10. Ndugu Harrison Mwakyembe
11. Ndugu January Makamba
12. Ndugu Amina Makillagi
13. Ndugu Christopher Ole Sendeka
14. Ndugu Stephen Wasira
15. Ndugu Abdallah Bulembo
16. Ndugu Hadija Aboud
17. Ndugu Mohamed Aboud
18. Ndugu Lazaro Nyalandu
19. Ndugu Issa Haji Ussi
20. Ndugu Waride Bakari Jabu
21. Ndugu Mahmoud Thabit Kombo
22. Ndugu Shamsi Vuai Nahodha
23. Ndugu Maua Daftari
24. Ndugu Stephen Masele
25. Ndugu Pindi Chana
26. Ndugu Shaka Shaka
27. Ndugu Makongoro Nyerere
28. Ndugu Bernard Membe
29. Ndugu Sadifa Juma Khamis
30. Ndugu Antony Diallo
31. Ndugu Livingston Lusinde
32 . Ndugu Ummy Mwalimu


Imetolewa na:-

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527