ANGALIA PICHA- JINSI MHESHIMIWA LOWASSA ALIVYORUDISHA FOMU YA URAIS JIJINI DAR ES SALAAM

Mheshimiwa Edward Lowassa leo  amerejesha fomu ya kugombea urais CHADEMA na mwenyeji wake Makamu Mwenyekiti bara wa CHADEMA Prof Abdallah Safari amepokea fomu hizo.

Prof Safari amesema mpaka sasa hakuna mgombea yoyote wa Chadema zaidi ya Mheshimiwa Edward Lowassa aliyechukua fomu ya kugombea Urais.
Mheshimiwa Edward Lowassa amedhaminiwa na wanachama zaidi ya milioni 1 na laki 6

Makamu Mwenyekiti akipokea fomu kutoka kwa Waziri Mkuu Mstaafu na aliyekuwa mbunge wa Monduli kwa tikeki ya CCM Mh. Edward Lowassa



Mwanasheria wa Chama Mh Mabere Marando akikagua fomu za mgombea urais Mh. Edward Lowassa mara baada tu ya kukabidhi kwa Makamu Mwenyekiti Bara Prof Abdalah Safari



Naibu Katibu Mkuu Zanznibar Mh Salum Mwalim akimkaribisha Edward Lowassa katika ofisi ya Makamu Mwenyekiti Bara Prof Abdalah Safari
Baadhi ya wabunge walioweza kufika katika tukio la kumshuhudia Edward Lowassa akirudisha fomu Makao Makuu


Ester Bulaya akiwa ukumbini kumshuhudia Edward Lowassa akirudisha fomu ya kugombea urais ndani ya chama



Viongozi mbalimbali wa Chadema



Mfuasi wa Lowasa akiwa amebeba bango

Suzan Lyimo Mbunge viti maalum CHADEMA akisalimiana na Mh Edward Lowassa mara baada ya kuwasili Makao Makuu kurudisha fomu ya kugombea urais kupitia CHADEMA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527