|
Hapa ni katika viwanja vya Mahakama ya Mwanzo Nguzo Nane
mjini Shinyanga ambapo leo jioni mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema pamoja
na mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA)
taifa Patrobas Katambi wamehutubia maelfu ya wakazi wa Shinyanga na kutoa elimu
ya uraia.Pamoja na mambo mengine Gobless Lema amewataka Watanzania kubadilika
na kuacha tabia ya Uoga katika kufanya maamuzi magumu ikiwemo kuwaondoa
madarakani viongozi wasio waadilifu-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
|
|
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chama Cha Demokrasia na
Maendeleo(BAVICHA) taifa Patrobas Katambi akizungumza katika mkutano huo ambapo alitangaza rasmi nia kugombea ubunge wa jimbo la
Shinyanga Mjini Kupitia UKAWA katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Katambi alisema yeye ni mzaliwa wa Shinyanga hivyo atakomaa katika jimbo la Shinyanga
Mjini kuhakikisha anagombea ubunge ili kuondoa uongozi wa Chama Cha Mapinduzi
ambao umekuwa ukifanya ubadhirifu wa fedha na kutowaletea maendeleo wananchi.Baada ya kutangaza nia hiyo Umati wa watu ukapiga kelele nyingi wakiashiria kuwa walikuwa wanamsubiri kwa hamu atamke kuwa atagombea kwani anaonekana kuwafaa wakazi wa Shinyanga
|
“Mimi ni mtu wa Shinyanga,Natangaza rasmi kuwa nitagombea ubunge katika jimbo la Shinyanga Mjini,uwezo ninao na nia ninayo,naungana na watangaza nia wengine waliotangulia,naomba ushirikiano tu,kama jina langu litapitishwa tutafanya mambo makubwa katika jimbo hili, kwani
najiamini na najua ninachokifanya,na siku zote mti wenye matunda ndiyo
unaopigwa mawe,mimi naamini katika haki zaidi na kufuata sheria za nchi,mwaka huu lazima kieleweke”,alieleza Katambi.
|
Wakazi wa Shinyanga wakifuatilia kilichokuwa kinajiri eneo la mkutano.“Sijajipitisha kugombea,bali nitafuata taratibu za Chama
changu,nitaandika barua kupeleka jina langu ili kusimikwa kuwa mgombea wa
ubunge na endapo atapitishwa mtu mwingine zaidi yangu,tutamuunga mkono kwani
chama chetu ni cha Umoja na tunafanya kazi moja ya kuleta ukombozi kwa
wananchi”,alieleza Katambi.
|
|
Kushoto ni Mtangaza nia ya Ubunge Shinyanga Mjini Patrobas Katambi akiwa na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema ambaye naye alijigamba kuwania ubunge katika jimbo lake.
Wakazi wa Shinyanga wakifurahia baada ya kusikia kuwa Bwana Patrobas Katambi kuwa atawania ubunge katika jimbo la Shinyanga mjini ambalo sasa linaongozwa na mbunge wa CCM ndugu Stephen Masele |
|
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akizungumza na wakazi wa Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine amewataka
watanzania Kumpuuza kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe kwa madai
kuwa amepewa pesa na CCM ili azunguke nchi nzima kuvuruga Chadema(UKAWA) lakini
akasisitiza kuwa Kamwe Hataweza kwani wameshajua anachokifanya ndiyo maana
kwenye mikutano yake hathubutu kuisema vibaya CHADEMA na maeneo aliyothubutu
wananchi wamekuwa wakimzomea. |
|
Godbless
Lema pia alivitaka vyombo vya ulinzi na usalama nchini kufanya kazi kwa
kuzingatia sheria za nchi badala ya kupendelea chama Tawala. |
|
Mbunge Lema pia alisema Kitendo cha Zitto Kabwe kujitangaza kuwa ni Mzalendo ni Unafiki Mtupu kwani Uzalendo haupimwi kwa Umaskini kwani hakuna mtu anayependa kuwa maskini kila mtu anapenda kuwa na maisha mazuri. |
|
Mkutano unaendelea-Lema pia alidai kuwa Matatizo mengi yaliyopo nchini Tanzania siyo CCM bali ni Uoga wa Watanzania wenyewe kufanya maamuzi magumu |
|
Jukwaa kuu wakifuatilia kilichokuwa kinajiri kwenye mkutano |
|
Mkutano unaendelea |
|
Jukwaa kuu wakifuatilia hotuba ya mheshimiwa Godbless Lema |
|
Wakazi wa Shinyanga wakiwa eneo la mkutano |
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde blog
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527