Mahakama ya wilaya ya Tabora imehukumu Masudi Nassoro mkazi wa kata ya Kiloleni manispaa ya Tabora (20) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya ulawiti kwa mwanafunzi wa kike wa shule ya msingi mwenye umri wa miaka 9.
Akitoa hukumu hiyo hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Tabora
mjini,Bahati Chitepo amesema kwamba ametoa adhabu hiyo ili iwe
fundisho kwa watu wengine wenye nia kama hiyo kwa watoto, na jamii
ijifunze kutoka kwake.
Awali mwendesha mashitaka wakili wa serikali Miradi Kijulu
amesema kuwa mshitakiwa Masoud Nasoro alitenda kosa hilo eneo la kata
ya Kiloleni ambapo muathirika wa tukio hilo alimuomba lifti akiwa
anakwenda shuleni na ndipo mshitakiwa alimpeleka vichakani mtoto huyo
eneo la Kalunde na kumfanyia unyama huo.
Baada ya kutenda kosa hilo mshitakiwa alikimbia hadi alipotiwa
nguvuni na jeshi la polisi na kufikishwa mahakamani.
Hata hivyo
mshitakiwa huyo aliiomba mahakama hiyo impunguzie adhabu kwani anaishi
na babu yake mlemavu wa mguu na wazazi wake wote wamafariki dunia,
maombi ambayo yaliyupiliwa mbali.
Via>>ITV
Via>>ITV