Mwonekano wa mikono ya bibi huyo iliyoonekana kama imekatwa kwa mapanga na imekomaa kwa nyuma-picha na Kadama Malunde
Malunde1 blog iliyofika eneo la tukio haraka iwezekanavyo
kama kawaida yake imeambiwa kuwa bibi huyo ambaye hakujulikana jina wala makazi yake
awali alikuwa haongei na aliposemeshwa ndipo akaanza kuongea kwa lugha ya
Kisukuma maneno yasiyoeleweka huku akisikika akisema wenzake wamemuacha alikuwa
anaenda kwenye sherehe-picha na Kadama Malunde-Shinyanga
Hatimaye bibi akaweza kusimama na kuanza kufanya vituko vya kila aina-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Bibi akaamua kukaa na kuanza kutoa pesa alizokuwa amezifunga kiunoni kwa kwenye mfuko wa rambo laini uliokuwa umefungwa kitaalam-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Bibi akiangalia pesa zake-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Zilikuwa ni shilingi za hamsini hamsini,mia moja ,mia mbili,mia tano na elfu akaziweka kwenye kibakuli kilichokuwa eneo la tukio -picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Kushoto ni mjumbe wa serikali ya mtaa wa Mageuzi Waziri Musa(CHADEMA) akisaidiana na wananchi wa eneo hilo kumwondoa bibi huyo kwenye nyumba ya mkazi wa eneo hilo -picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Bibi akawekwa chini ya mti,hata hivyo akaendelea kufanya vituko na kuamua kulala juu ya mawe,angalia hapa chini-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Bibi akiwa amelala juu ya mawe kabla askari polisi hawajafika eneo la tukio leo mchana japokuwa bibi huyo amekutwa nyumbani kwa mtu saa moja asubuhi-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Askari polisi wakimwangalia bibi huyo-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Askari polisi wakitoa maelekezo kwa wananchi wa mtaa huo ambapo walisema serikali haiamini ushirikina hivyo kuwataka wananchi waondoke eneo la tukio na kumwacha bibi aendelee na safari yake kwani tayari alikuwa amepata nguvu na kuanza kutembea kwa miguu badala ya makalio kama mwanzo-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |
Askari polisi akiwa amembeba bibi huyo kumtoa kwenye mawe,na katika hali ya kushangaza bibi huyo alimng'ang'ania askari huyo.Mpaka malundeq blog inaondoka eneo la tukio saa 14:10pm wakazi wa Mageuzi walikuwa wameanza kutawanyika huku bibi huyo akiondoka katika mtaa huo-picha na Kadama Malunde-Shinyanga |