Hekaheka za Chrismas!! MKE WA MTU ANASWA AKIJIUZA APATE PESA YA SIKUKUU



Morogoro Ni aibu iliyoje! Tabia ya wanawake kujiuza kwa kisingizio cha kusaka fedha kwa ajili ya Sikukuu ya Krismasi imewatokea puani wanawake zaidi ya kumi akiwemo mke wa mtu baada ya kunaswa mawindoni na kutiwa nguvuni.
 
Tukio hilo la aibu lilitokea katika msako maalum wa polisi waliotoa kolabo kwa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, uliofanyika katika eneo ‘korofi’ la ltinga, Msamvu Kata ya Mwembesongo mkoani Morogoro, wikiendi iliyopita.

Awali, Kamanda wa OFM mkoani hapa alipokea malalamiko lukuki kutoka kwa wananchi waishio jirani na eneo hilo waliokuwa wakiwalalamikia wanawake hao kugeuza vibanda vyao vya simu kuwa gesti na kuvitumia kufanyia ngono usiku na kuzagaa kwa kondom kila sehemu.

Mke wa mtu (wa kwanza kushoto) akijificha kwa aibu.

Kabla ya msako, OFM iliwashauri kupeleka malalamiko hayo kwenye serikali ya mtaa na polisi.

Kabla ya kufanya oparesheni hiyo, shushushu wetu alifanya upelelezi na kubaini kwamba ni kweli wanawake hao huvitumia vibanda hivyo kama gesti.

Baada ya kujiridhisha, OFM na jeshi la polisi walipofika eneo hilo majira ya saa 5:00 usiku na kuwanasa wanawake hao kisha kuwasukumiza kwenye difenda na kwenda kuwasweka lupango kusubiri sheria ichukue mkondo wake.

...Wakitupiwa kwenye difenda ili kuchukuliwa hatua za kisheria.

Katika hali ya kushangaza, mmoja wa wanawake hao alikuwa akiomba msamaha kwa madai kwamba ni mke wa mtu hivyo mumewe akijua ishu hiyo atamtoa roho.

“Jamani mimi ni mke wa mtu, mume wangu alivyo mkali akijua nimekutwa huko atanimaliza,” alisikika mwanamke huyo.

Stori na Dustan Shekidele-Morogoro

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527