VIONGOZI WA CHADEMA SHINYANGA WAHAMIA CHAMA KIPYA CHA ACT

Godwin Makomba,mmoja wa viongozi waliohama Chadema

Chama kipya Cha Aliance for Change and Transparent (ACT), Tanzania kimenza kuonesha makucha yake mkoani Shinyanga baada ya viongozi wa Chadema kujivua nyadhifa zao na kuhamia chama hicho kwa madai kuwa rushwa imetawala ndani ya Chadema

Waliojivua nyadhifa zao na kujiunga na ACT ni Godwin Makomba, aliyekuwa katibu wa chadema jimbo la Solwa katika halmashauli ya wilaya ya Shinyanga vijijini na mjumbe wa mkutano mkuu wa wilaya,Merikioli Sebastiani, aliyekuwa katibu mwenezi wa kata ya Kambarage, Samweli Dalla aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema wa kata ya Kambarage  wilaya ya Shinyanga Mjini na Samweli Rafael  aliyekuwa mhasibu wa kata ya Kambarage. 

Wamesema wameamua kujiunga na ACT kutokana na Chama chao cha awali (Chadema),kutowatendea haki na kutozingatia Demokrasiana viongozi wa ngazi za juu kudharau viongozi wa ngazi za chini na kwamba baadhi ya taarifa za kiofisi zinazowahusu zilikuwa haziwafikii.

“Tumeamua kujivua uanachama kwani viongozi wa ngazi ya juu wamekuwa wakikemea rushwa na kudai demokrasia  hasa kwenye uchaguzi wa ndani ya chama uliopita  baadhi ya majina ya watu yalichakachuliwa  manispaa na kuingizwa majina ambayo hayakutakiwa  kwa hilo tutaonekana wanafiki kwa kutoendana na kauli zinazotamkwa”waliiambia Malunde1 blog

Wamesema baadhi ya walioenguliwa bila sababu yoyote kwa mizengwe na kupitia kura za red-brigde  ni aliyekuwa mwenyekiti wa wilaya wa chama hicho na diwani viti maalumu Siri  Yasin na diwani wa kata ya Kambarage (Chadema) ,aliyekuwa  katibu wa mkoa  na baraza la wazee taifa Nyangaki Shilungushela.

Mwenyekiti wa ACT, wilaya ya Shinyanga Mjini Suleimani Masoud amethibitisha kuwapokea wanachama hao wapya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527