HII NDIYO NYAMA ALIYOKULA MWATHIRIKA WA KWANZA WA EBOLA


Nyama wa wanyama wa msituni ndio inaaminika kuwa chanzo cha mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola ambao umekuwa janga kwa mataifa kadhaa ya Afrika Magharibi na kwa ulimwengu wote.
Familia ya Mwathiriwa wa kwanza wa Ugonjwa huo iliwinda Popo ambao huwa na virusi vya Ebola.
Lakini katika baadhi ya wanyama hawa huwa wamebeba magonjwa hatari.
Kama Popo huwa wamebeba virusi aina tofauti ambavyo ni hatari kwa mwili wa binadamu huku baadhi ya Popo wanaokula matunda wakiwa na virusi vya Ebola.
Nyama ya wanyamapori ambayo huchomwa au kupikwa huwa haina athari sana mwilini
Kinyesi cha wanyama hao kilicho na virusi hivyo kinaweza kuwaathri wanyama wengine kama vile Nyani na Sokwe.
Kwa wanyama hao kama kwa binadamu virusi hivyo vinaweza kuwa hatari.
Lakini Popo wanaweza wasiathirike sana.
Kwa hivyo inakuwa rahisi kwao kubeba virusi hivyo bila ya kuathirika kwa vyovyote.
Raia wengi wa Afrika Magharibi hula nyama ya wanyama wa msituni
Je ulaji wa nyama ya wanyama wa msituni inaweza kuwa ndio chanzo cha janga la Ebola ambalo limekumba hasa kanda ya Afriak Magharibi?
Kitovu cha janga hilo kimesemekana kuwa mtoto mwenye umri wa miaka miwili kutoka kijiji cha Gueckedou Kusini Mashariki mwa Guinea, eneo ambalo nyama Popo ambayo huwindwa na kuliwa mara kwa mara.
Mtoto huyo aliyesemekana kuitwa, Child Zero, alifariki tarehe sita Disemba mwaka 2013.
Hata hivyo haijulikani ambavyo virusi hivyo vinaathiri mwili wa binadamu, kulingana na Profesa Jonathan Ball,mtaalamu wa virusi katika chuo kikuu cha Nottingham.
Nyama hiyo huuzwa katika masoko mengi katika eneo hilo
Anasema inawezekana virusi hivyo hupitia kwa wanyama kama Nyani lakini ushahidi unaonyesha kuwa virusi hivyo pia vinaweza kupitia kwa Popo.
Hata hivyo anasema ni vigumu kwa virusi kutoka kwa mnyama hadi kwa binadamu.
Anasema mwanzo virusi vinaingia kwa seli za mwili ambapo vinazaana kwa kuugusana na damu mwilini.
Zaidi ya Popo 100,000 huliwa nchini Ghana kila mwaka
Familia ya mtoto huyo,ilisema kuwa iliwinda aina mbili ya Popo ambayo huwa na virusi vya Ebola.
Nyama ya msituni inaweza kutoka kwa Nyani, Popo wanaokula matunda na wakati mwingine hata kutoka kwa Panya na Nyoka.
Kutoka katika maeneo mengine nyama hii huwa ni mlo muhimu kwa jamii lakini kwa wengine hula tu kama njia ya kufurahisha nafsi zao.
Nchini DRC watu hula milioni ya tani za nyama ya wanyama wa msituni kwa mujibu wa shirika la utafiti la (Centre of International Forestry Research,) kila mwaka.
Popo wanaokula Marunda wanaaminika kubeba virusi vya Ebola lakini huwa wahaonyeshi dalili za kuambukizwa virusi hivyo
Sio nchini DRC pekee ambako nyama ya wanyama wa msituni huliwa bali pia nchini Ghana.
Lakini cha kushangaza ni kwamba hapajakuwa na hata kisa kimoja cha maambukizi ya Ebola nchini Ghana.
via>>BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527