TAZAMA PICHA-JAMAA ANASWA AKITAKA KUBAKA MTOTO SHINYANGA ,APEWA KIPIGO CHA MBWA MWIZI


Pichani ni jamaa/mwanamme ambaye hakujulikana jina wala makazi yake aliyenusurika kufa kutokana na kipigo cha wananchi wenye hasira kali baada ya kudaiwa kukuktwa akifanya jaribio la kutaka kumbaka mtot o mwenye umri wa miaka mitano jioni ya leo eneo la kata ya Masekelo katika manispaa ya  Shinyanga.Tukio hili linakuja siku moja tu baada ya mazishi ya mtoto Happiness Kashinje mwenye umri wa miaka 9 kubakwa,kutobolewa macho kisha kuuawa na watu wasiojulikana katika kata jirani ya tukio la leo ya Ndala
Inaelezwa kuwa Jamaa huyu kakamatwa na wananchi mida ya saa 11,jioni lakini mpaka saa moja usiku alikuwa bado anapewa kipigo na wananchi hao,hadi pale jeshi la polisi lilipofika kuokoa maisha yake
Walioshuhudia tukio hilo wanasema Jamaa huyu kakutwa akimchezea sehemu za siri mtoto nje ya nyumba karibu na choo,na kufuatia kelele za mtoto huyo ndipo ndipo wasamaria wema wakaanza kumpa kipigo jamaa huyo

 Mawe fimbo n.k,Wananchi wenye hasira wakiwa katika harakati za kumwadhibu jamaa huku viongozi wa mtaa na sungusungu wakizuia asipigwe
Ni katika eneo la tukio

Umati wa wananchi wakiwa eneo la tukio

Mmoja kati hawa watoto wawili kanusurika kufanyiwa unyama na jamaa aliyepigwa na wananchi wenye hasira jioni hii mjini Shinyanga(Jina la mtoto linahifadhiwa na Malunde1 blog kwa sababu za kimaadili)

Wananchi wakiwa na hasira
Viongozi wakizuia jamaa anayedaiwa kutaka kubaka mtoto asipigwe kwani wananchi walitaka kumchoma moto


Pichani ni jamaa/mwanamme ambaye hakujulikana jina wala makazi yake aliyenusurika kufa kutokana na kipigo cha wananchi wenye hasira kali baada ya kudaiwa kukuktwa akifanya jaribio la kutaka kumbaka mtot o mwenye umri wa miaka mitano jioni ya leo eneo la kata ya Masekelo katika manispaa ya  Shinyanga
Baada ya jeshi la polisi kufika
 Baada ya askari polisi kufika eneo la tukio,jamaa anapelekwa kwenye gari la polisi


Tayari kapanda kwenye gari la polisi,usiku huu

Polisi wanaondoka na mtuhumiwa wa ubakaji

Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527