MGANGA WA JADI ADAIWA KUMKATA MKONO ALIBINO HUYU AKIWA NA WENZAKE KISHA KUTOKOMEA KUSIKOJULIKANA NA MKONO HUO


Ukatili dhidi ya wenye ulemavu wa ngozi (Albino) umejitokeza tena mkoani Tabora ambapo mtoto Pendo Sengerema (14) mwanafunzi wa darasa la sita shule ya msingi Nundu, amekatwa mkono wake wa kulia na wahalifu kukimbia nao kusikojulikana na aliyeshiriki uharifu huo akihaidiwa kulipwa laki tisa huko katika kijiji cha Usinge wilayani Kaliua.

Akiongea kwa tabu alipolazwa katika hospitali ya wilaya ya Urambo mkoani Tabora majeruhi Pendo Sengerema amesema kuwa, aliyemkata mkono alimfahamu maana ni jirani anayesadikiwa kuwa, ni mganga wa kienyeji, ambapo kaimu mganga wa hospitali hiyo, Dokta James Kang’oma, akidai kuwa walijitahidi kuokoa maisha yake kutokanana kutoka kuvuja damu nyingi.

Mratibu wa chama cha wenye ulemavu wa ngozi wilaya za Urambo na Kaliua Bw Focus Mgesera, amesema kuwa, pamoja na mtoto huyo kulazwa katika hospitali hiyo bado kuna hali ya hatali kwake kwani kwa namna moja ama nyingine anaweza kuuawa kutokana na kuwafahamu waliomjeruhi, hivyo anahitaji ulinzi.

Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Under the same sun, Bi Vicky Ntetemya aliyefika hospitalini hapo kumwona mtoto huyo amesema kuwa, serikali iwe makini na jamii ya wenye ulemavu wa ngozi kutokana na masuala ya wagombea nafasi za uongozi kujishirikisha ma mambo ya waganga wa kienyeji.

Chama cha walemavu wa ngozi nchini kimeraani tukio hilo kikitaka serikali kuongeza ulinzi kwa jamii hiyo ambapo akizungumza kwa njia ya simu, kamanda wa polisi mkoani Tabora Suzan Kaganda akidhibitisha kutokeaa tukio hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post