MWENYEKITI WA KIJIJI ATUPWA JELA KWA KUTISHIA KUUA HUKO GEITA

Mahakama ya wilaya Geita  mkoani Geita imemhukumu mwenyekiti wa kijiji cha Katoro Joeri Mazemre msukuma  (42) kwenda jela miezi sita na kulipa faini ya shilingi laki 2 ,baada ya kupatikana na kosa la kutishia kuua.
Akisoma shtaka hilo jana mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo Desdery Kamugisha mwendesha mashitaka wa Serkali Zephania  Juma  alisema mnamo tarehe 8.5 2002 majira ya saa nane katika kijiji cha Katoro mshitakiwa Joel Mazemle alitishia kumuua Samwel Mashili mkazi wa Katoro.
Mwendesha mashtaka aliendelea kuilezea mahakama kuwa mshitakiwa alikuwa na ugomvi wa shamba na mlalamikaji hali iliyosababisha mshtakiwa asijihusishe na kusuruhisha mgogoro huo kwa kuwa yeye alikuwa kiongozi wa kijiji.
Alisema uongozi wa baraza la ardhi la kata waliamua kwenda kusuruhusha mgogoro huo lakini katika hali ya kushangaza baada ya kufika walimkuta mshtakiwa akiwa kwenye shamba hilo akiwasubiri.

Mshtakiwa alipowaona alianza kumtishia mlalamikaji kwamba atamuua kutokana na kwamba anataka kudhurumu shamba lake.

Kufuatia hali hiyo ndipo uongozi wa baraza hilo ulipoagiza polisi kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha kituo cha Polisi.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu mwendesha mashtaka huyo aliiomba mahakama kutoa hukumu kali  ili liwe fundisho kwa wengine kutokana na kitendo cha kutishia kuua kutokubalika katika katika jamii iliyostaarabika.
Baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka hvyo kuhukumiwaa hivyo kuhukumiwa kwenda jela miezi 6 na kumlipa mlalamikaji shilingi laki mbili.

Na Valence Robert-Malunde1 blog-Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527