MTOTO WA MIAKA 6 ACHOMWA MOTO MIGUU YOTE NA MAMA YAKE MZAZI

 Miguu ya mtoto Brayan iliyochomwa na mama yake mzazi.


MTOTO, Brayani Emanuel mwenye umri wa miaka sita, amenusurika kuuawa baada ya mama yake mzazi Rose Mwanisisi Mkazi wa kitongoji cha Chemchem kilichopo eneo la Mbalizi Mbeya vijijini, kujaribu kumchoma moto kwa kutumia mifuko ya manila.

Tukio hilo limetokea Julai 16 mwaka huu, ambapo imeelezwa kuwa mama huyo baada ya kurudi nyumbani kwake majira ya jioni hakumkuta mtoto,hivyo aliaanza kumtafuta na alipompata alimfungia ndani na kisha kumchoma  moto kwa kutumia mifuko ya manila.

Mtoto huyo ambaye kwa sasa analelewa na Babu yake Emanuel Omary(61), alisema mama yake alipomkamata alimuingiza ndani kisha alichukua mifuko ya rambo(manila) na kumuwekea kwenye miguu yake.

Aliendelea kufafanua kuwa, baada ya mama huyo kuweka mifuko ya rambo kwenye miguu alienda kuchukua kibatari na kuanza kuunguza mifuko hiyo kwenye miguu yake licha ya mtoto huyo kuomba msamaha.

“Mama alinikuta ninacheza na wenzangu  mbali kidogo na eneo la nyumbani, alinichukua  na tulipofika nyumbani aliniambia kwamba amechoka na mimi hivyo leo atanifundisha adabu, ndipo alichukua mifuko ya rambo na kibatari na kuanza kuniunguza kwenye miguu yangu,”alisema mtoto huyo.



Amesema, wakati mama yake akiendelea na zoezi hilo la kumuunguza miguu kwa kutumia uji wa moto uliotokana na kuungua kwa mifuko hiyo ya manila yeye aliendelea kupiga kelele za kuomba msamaha mpaka majirani walivyofika na kumuokoa.

via>> Fahari News

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527