ANGALIA PICHA SIKUKUU YA IDD EL FITR LEO ASUBUHI MJINI SHINYANGA


Hapa ni katika viwanja vya sabasaba mjini Shinyanga ambako leo kumefanyika swala ya IDD EL FITR ambayo imehudhuriwa pia na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga

Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika viwanja vya sabasaba katika  mjini  Shinyanga kwa ajili ya kuswali swala ya Idd el-fitr leo
Sherkhe wa mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akizungumza na waumini wa kiislamu katika viwanja vya saba saba mjini Shinyanga
Sheikh wa mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akizungumza na waumini wa dini ya kiislamu mara baada ya kumaliza kuswali swala ya Idd el- fitri,ambapo aliwataka kuendelea kuiombea nchi ili amani iliyopo iendelee kuwepo sanjari na mchakato wa kupata katiba mpya umalizike kwa amani na kuwepo maelewano kwa wajumbe wa bunge maalumu la katiba. 
 Waislamu wakiwa katika viwanja vya sabasaba mjini Shinyanga leo
                
Sheikh wa wilaya ya Shinyanga  Sudy Suleiman akitoa wito  kwa waislamu wote kujibidisha katika  elimu hasa kwa watoto ,ambapo alisema ukitaka kuishi salama katika  dunia na ahera  lazima usome kama alivyohusiwa na  mtume   Mohamad  S.W.A na mwenyezi mungu.

Sheikh Sudy Suleiman akiendelea kuzungumza
Mkurugenzi wa Shalleyhabari blog pia mwandishi wa habari Star tv/RFA bwana Shaban Alley akichukua matukio katika viwanja vya sabasaba mjini Shinyanga leo

Waumini wa dini ya kiislam wakifuatilia kilichokuwa kinajiri uwanjani

Kushoto ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga ndugu Ally Nassoro Rufunga akiwa katika viwanja vya sabasaba leo 

Viongozi katika picha ya pamoja
Ni katika viwanja vya sabasaba leo
Waumini wa dini ya kiislamu wakitoka katika viwanja vya sabasaba baada ya kuswali swala ya Idd el fitri leo.
Trafiki wakiangalia usalama wa rai katika kuhakikisha kila kitu kinaenda vizuri.

Picha zote kwa hisani ya Shalleyhabari blog na Stella blog


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527