Msaada!! TAZAMA PICHA MGONJWA ALIYEOZA MAKALIO KISHA KUTIMULIWA BUGANDO,TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI

Hali halisi ya makalio ya Joseph Luhogola (38),mkazi wa Kitongoji cha Nyabugera,Kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato katika Mkoa wa Geita ambapo Hospitali ya rufaa ya Bugando ya Jijini Mwanza baada ya kudaiwa kumtimua Mgonjwa wake ambaye ameozea Wodini hapo na sasa anaendelea kuoza akiwa nyumbani kwa mganga wa tiba za asili.

Joseph Luhogola (38),mkazi wa Kitongoji cha Nyabugera,Kijiji cha Mganza Wilaya ya Chato katika Mkoa wa Geita akiwa amelala nyumbani kwa mganga wa tiba za asili Paul Chasama ambaye ni mtaalamu wa tiba za jadi kwa  kuunga mifupa na kurudisha viungo vya mwili vilivyochengana ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha Elimu,katika kijiji cha Nyankumbu Wilayani Geita amedai kuwa,kutokana na uzoefu kwenye kazi hiyo anao uhakika wa asilimia mia kwamba Luhogola atapona.

Baadhi ya watu wamedai iwapo mganga Chasama atafanikiwa kumponya kijana huyo aliyeoza makalio yake kama unavyoona pichani basi watalazimika kuwaondoa wagonjwa wao hospitali na kuwapeleka kwake.Picha zote na Victor Bariety-Geita

Kama umeguswa na habari hii ya kusikitisha wasiliana na mwandishi wa Malunde1 Blog mkoani Geita ndugu Victor Bariety kwa simu namba 0763 681 747 kwa ajili ya msaada kwa mgonjwa aliyeoza makalio ndugu Joseph Luhogola




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527