UNAFIKIRI NANI ATAWATETEA HAWA?? WANANYANYASIKA KILA KUKICHA


Bado maeneo ya mikoa ya Shinynga na Simiyu imeonekana kuwa wakazi wake wana tabia ya kuwanyanyasa wanyama kama inavyojieleza katika picha ambapo kamera za mtandao huu wa malunde1 blog ziliwanasa wanyama hawa aina ya punda wakiwa wamebebeshwa mizigo mizito zikiwemo injini za gari,matairi na vyuma mbalimbali kinyume na taratibu za haki za wanyama katika kijiji cha Wigelekelo wilaya ya Maswa mkoa mpya wa Simiyu.


Wanyama wameendelea kunyanyaswa wakati asasi nyingi za kutetea haki za wanyama kama vile Tanzania Animals Pritection Organisation (TAPO)yenye makao yake jijini Dar es salaam na ofisi yake iliyopo Kahama mkoani Shinyanga na wahusika wengine wengi wakiwa wamekaa kimya. Ng'ombe,mbwa,punda,paka na hata ndege wafugwao wamekuwa wakinyanyasika kwa kupigwa,kutopata huduma za afya,kubebeshwa mizigo mizito,kutopewa chakula.


Je ni nani atakayewatetea wanyama hawa!??

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments